MASOMO
SOMO 1:
SOMO 1:
Mwa.21:5,8-20
Ibrahimu alikuwa mtu wa miaka mia, alipozaliwa mwana wake Isaka. Mtoto akakua, akaachishwa kunyonya; Ibrahimu akafanya karamu kuu siku ile Isaka alipoachishwa kunyonya. Sara akamwona yule mwana wa Hajiri Mmisri, ambaye alimzalia Ibrahimu, anafanya dhihaka. Kwa hiyo akamwambia Ibrahimu, Mfukuze mjakazi huyu na mwanawe, maana mwana wa mjakazi hatarithi pamoja na mwanangu, Isaka. Na neno hilo lilikuwa baya sana machoni pa Ibrahimu, kwa ajili ya mwanawe. Mungu akamwambia Ibrahimu, Neno hili lisiwe baya machoni pako, kwa ajili ya huyo mwana, na huko mjakazi wako. Kila akuambialo Sara, sikiza sauti yake, kwa maana katika Isaka uzao wako utaitwa. Naye mwana wa mjakazi nitamfanya kuwa taifa, maana huyu naye ni uzao wako. Ibrahimu akaamka asubuhi na mapema akatwaa mkate na kiriba cha maji, akampa Hajiri akimtwika begani pake, na kijana, akamruhusu; naye akatoka, akapotea katika jangwa la Beer-sheba. Yale maji yakaishaisha katika kiriba, akamlaza kijana chini ya kijiti kimoja. Akaenda akakaa akimkabili, mbali i kadiri ya mtupo wa mshale; maana alisema, Nisimwone kijana akifa; naye akakaa akimkabili, akapazaza sauti yake, akalia. Mungu akasikia sauti ya kijana. Malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, Una nini, Hajiri? Usiogope, maana Mungu amesikia sauti ya kijana huko aliko. Ondoka, ukamwinue kijana, ukamshike mkononi mwako, kwa kuwa nitamfanya kuwa taifa kubwa. Mungu akamfumbua macho, naye akaona kisima cha maji; akaenda akakijaza kiriba maji, akamnywesha kijana. Mungu akawa pamoja na huyo kijana, naye akakua, akakaa katika jangwa, akawa mpiga upinde.
WIMBO WA KATIKATI: Zab.34:6-7,9-13 (K)6
1. Maskini huyu aliita, Bwana akasikia, Akamwokoa na taabu zake zote. Malaika wa Bwana hufanya kituo, akiwazungukia wamchao na kuwaokoa.
(K) Maskini huyu aliita, Bwana akasikia.
2. Mcheni Bwana, enyi watakatifu wake, yaani, wamchao hawahitaji kitu. Wana-simba hutindikiwa, huona njaa, bali wamtafutao Bwana hawatahitaji kitu chochote kilicho chema. (K)
3. Njoni, enyi wana, mnisikilize, nami nitawafundisha kumcha Bwana. Ni nani mtu yule apcndezwaye na uzima, apendaye siku nyingi apate kuona mema? (K)
SHANGILIO: Zab.119:105
Aleluya, aleluya!
mungu alikuwa ndani ya Kristu,
Neno lako ni taa ya miguu yangu,
na mwanga wa njia yangu.
Aleluya!
INJILI:
Ibrahimu alikuwa mtu wa miaka mia, alipozaliwa mwana wake Isaka. Mtoto akakua, akaachishwa kunyonya; Ibrahimu akafanya karamu kuu siku ile Isaka alipoachishwa kunyonya. Sara akamwona yule mwana wa Hajiri Mmisri, ambaye alimzalia Ibrahimu, anafanya dhihaka. Kwa hiyo akamwambia Ibrahimu, Mfukuze mjakazi huyu na mwanawe, maana mwana wa mjakazi hatarithi pamoja na mwanangu, Isaka. Na neno hilo lilikuwa baya sana machoni pa Ibrahimu, kwa ajili ya mwanawe. Mungu akamwambia Ibrahimu, Neno hili lisiwe baya machoni pako, kwa ajili ya huyo mwana, na huko mjakazi wako. Kila akuambialo Sara, sikiza sauti yake, kwa maana katika Isaka uzao wako utaitwa. Naye mwana wa mjakazi nitamfanya kuwa taifa, maana huyu naye ni uzao wako. Ibrahimu akaamka asubuhi na mapema akatwaa mkate na kiriba cha maji, akampa Hajiri akimtwika begani pake, na kijana, akamruhusu; naye akatoka, akapotea katika jangwa la Beer-sheba. Yale maji yakaishaisha katika kiriba, akamlaza kijana chini ya kijiti kimoja. Akaenda akakaa akimkabili, mbali i kadiri ya mtupo wa mshale; maana alisema, Nisimwone kijana akifa; naye akakaa akimkabili, akapazaza sauti yake, akalia. Mungu akasikia sauti ya kijana. Malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, Una nini, Hajiri? Usiogope, maana Mungu amesikia sauti ya kijana huko aliko. Ondoka, ukamwinue kijana, ukamshike mkononi mwako, kwa kuwa nitamfanya kuwa taifa kubwa. Mungu akamfumbua macho, naye akaona kisima cha maji; akaenda akakijaza kiriba maji, akamnywesha kijana. Mungu akawa pamoja na huyo kijana, naye akakua, akakaa katika jangwa, akawa mpiga upinde.
WIMBO WA KATIKATI: Zab.34:6-7,9-13 (K)6
1. Maskini huyu aliita, Bwana akasikia, Akamwokoa na taabu zake zote. Malaika wa Bwana hufanya kituo, akiwazungukia wamchao na kuwaokoa.
(K) Maskini huyu aliita, Bwana akasikia.
2. Mcheni Bwana, enyi watakatifu wake, yaani, wamchao hawahitaji kitu. Wana-simba hutindikiwa, huona njaa, bali wamtafutao Bwana hawatahitaji kitu chochote kilicho chema. (K)
3. Njoni, enyi wana, mnisikilize, nami nitawafundisha kumcha Bwana. Ni nani mtu yule apcndezwaye na uzima, apendaye siku nyingi apate kuona mema? (K)
SHANGILIO: Zab.119:105
Aleluya, aleluya!
mungu alikuwa ndani ya Kristu,
Neno lako ni taa ya miguu yangu,
na mwanga wa njia yangu.
Aleluya!
INJILI:
Mt.8:28-34
Yesu alipofika ng’ambo katika nchi ya Wagerasi, watu wawili wenye pepo walikutana naye, wanatoka makaburini, wakali mno, hata mtu asiweze kuipitia njia ile. Na tazama, wakapiga kelele, wakisema, Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu? Je! Umekuja kututesa kabla ya muhula wetu? Basi, kulikuwako mbali nao kundi la nguruwe wengi wakilisha. Wale pepo wakamsihi, wakisema, Ukitutoa, tuache twende, tukaingie katika lile kundi la nguruwe. Akawaambia, Nendeni. Wakatoka, wakaingia katika nguruwe; na kumbe! Kundi lote wakatelemka kwa kasi gengeni hata baharini, wakafa majini. Lakini wachungaji walikimbia, wakaenda zao mjini, wakazieneza habari zote, na habari za wale wenye pepo pia. Na tazama, mji wote ukatoka kwenda kumlaki Yesu; nao walipomwona, walimsihi aondoke mipakani mwao.
MAOMBI
Ndugu, si rahisi kuitekeleza amri ya mapendo kwa jirani, hasa pale zinapokuwepo tofauti baina ya wahusika, mintarafu uzao wa damu na usio wa damu. Tuombe neema ya Mungu tukisema:-
Kiitikio: Twakuomba utusikie. 1. Uwajalie Maaskofu na Mapadre wetu kushirikiana vema zaidi na watenda kazi wao, bila ubaguzi wa aina yoyote. Ee Bwana.
2. Wote wenye mamlaka wajaliwe roho ya kugawa madaraka na raslimali zilizopo, kwa njia za haki na amani bila upendeleo wowote ule. Ee Bwana.
3. Utujalie upendo wa kweli unaothamini na kuenzi zaidi uhai wa binadamu wenzetu, kuliko kitu kingine chochote. Ee Bwana.
4. Kila mmoja wetu ajibidishe kutafuta mema, wala si mabaya; kwani Wewe hupendezwi na ibada ya unafiki isiyoandamana na matendo mema. Ee Bwana.
5. Uwahurumie wagonjwa, wazee, wageni, yatima, wajane na wote wasiojiweza. Nao marehemu wetu wafikishwe mbinguni. Ee Bwana.
Ee Mungu uliyetuamshia mapendo ya kweli, uyapokee maombi yetu. Kwa njia ya Kristo Bwana wetu. Amina.
Yesu alipofika ng’ambo katika nchi ya Wagerasi, watu wawili wenye pepo walikutana naye, wanatoka makaburini, wakali mno, hata mtu asiweze kuipitia njia ile. Na tazama, wakapiga kelele, wakisema, Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu? Je! Umekuja kututesa kabla ya muhula wetu? Basi, kulikuwako mbali nao kundi la nguruwe wengi wakilisha. Wale pepo wakamsihi, wakisema, Ukitutoa, tuache twende, tukaingie katika lile kundi la nguruwe. Akawaambia, Nendeni. Wakatoka, wakaingia katika nguruwe; na kumbe! Kundi lote wakatelemka kwa kasi gengeni hata baharini, wakafa majini. Lakini wachungaji walikimbia, wakaenda zao mjini, wakazieneza habari zote, na habari za wale wenye pepo pia. Na tazama, mji wote ukatoka kwenda kumlaki Yesu; nao walipomwona, walimsihi aondoke mipakani mwao.
MAOMBI
Ndugu, si rahisi kuitekeleza amri ya mapendo kwa jirani, hasa pale zinapokuwepo tofauti baina ya wahusika, mintarafu uzao wa damu na usio wa damu. Tuombe neema ya Mungu tukisema:-
Kiitikio: Twakuomba utusikie. 1. Uwajalie Maaskofu na Mapadre wetu kushirikiana vema zaidi na watenda kazi wao, bila ubaguzi wa aina yoyote. Ee Bwana.
2. Wote wenye mamlaka wajaliwe roho ya kugawa madaraka na raslimali zilizopo, kwa njia za haki na amani bila upendeleo wowote ule. Ee Bwana.
3. Utujalie upendo wa kweli unaothamini na kuenzi zaidi uhai wa binadamu wenzetu, kuliko kitu kingine chochote. Ee Bwana.
4. Kila mmoja wetu ajibidishe kutafuta mema, wala si mabaya; kwani Wewe hupendezwi na ibada ya unafiki isiyoandamana na matendo mema. Ee Bwana.
5. Uwahurumie wagonjwa, wazee, wageni, yatima, wajane na wote wasiojiweza. Nao marehemu wetu wafikishwe mbinguni. Ee Bwana.
Ee Mungu uliyetuamshia mapendo ya kweli, uyapokee maombi yetu. Kwa njia ya Kristo Bwana wetu. Amina.
No comments
Post a Comment