MASOMO
SOMO 1:
SOMO 1:
Mwa.18:1-15
Bwana alimtokea lbrahimu karibu na mialoni ya Mamre, alipokuwa ameketi mlangoni pa hema yake mchana wakati wa hari, Akainua macho yake akaona, na tazama, watu watatu wamesimama mbele yake. Nave alipowaona alipiga mbio kuwalaki kutoka mlangoni pa hema, akainama mpaka nchi, akasema, Bwana wangu, kama nimeona fadhili machoni pako nakuomba usinipite sasa mimi mtumwa wako. Na yaletwe basi maji kidogo mkanawe miguu, mkapumzike chini ya mti huu. Nami nitaleta chakula kidogo, mkaburudishe moyo, baadaye mwendelee, iwapo mmemjia mtumwa wenu. Wakasema, Haya, fanya kama ulivyosema. Basi lbrahimu akaenda hima hemani kwa Sara, akasema, Himiza vipimo vitatu vya unga safi, uukande, ufanye mikate. lbrahimu akapiga mbio kwenda kundini, akaleta ndama wa ng’ombe aliye laini, mzuri, akampa mtumishi, naye akahimiza kuiandaa. Akatwaa siagi na maziwa, na ndama aliyoiandaa, akawaandikia mbele yao, akasimama karibu nao chini ya mti, nao wakala. Wakamwambia, Yu wapi Sara mkeo? Akasema, Yumo hemani. Akamwambia, Hakika nitakurudia wakati uu huu mwakani, na tazama, Sara mkeo atapata mwana wa kiume. Sara akasikia mlangoni pa hema iliyokuwapo nyuma yake. Basi lbrahimu na Sara walikuwa wazee, na umri wao mkubwa, na Sara alikuwa amekoma katika desturi ya wanawake. Kwa hiyo Sara akacheka moyoni mwake, akisema, Niwapo mkongwe, nitapata furaha, na bwana wangu mzee? Bwana akamwambia lbrahimu, Mbona Sara amecheka akisema, Mimi kweli nitazaa mwana, nami ni mzee? Kuna neno gani lililo gumu la kumshinda Bwana? Kwa muhula wake nitakurudia, wakati uu huu mwakani, na Sara atapata mwana wa kiume. Akakana Sara, akisema, Sikucheka, maana aliogopa. Naye akasema, Sivyo, umecheka.
WIMBO WA KATIKATI: Lk.1:46-50,53-55 (K)54
1. Moyo wangu wamwadhimisha Bwana. Na roho yangu imemfurahia Mungu Mwokozi wangu.
(K) Bwana alikumbuka rehema zake.
2. Unyonge wa mjakazi wake. Kwa maana, tazama, tokea sasa Vizazi vyote wataniita mbarikiwa. (K)
3. Kwa kuwa mwenye nguvu amenitendea makuu, Na jina lake ni takatifu. Na rehema zake hudumu vizazi hata vizazi, Kwa hao wanaomcha. (K)
4. Amemsaidia Israeli, mtumishi wake: Ili kukumbuka rehema zake. Kama alivyowaambia baba zetu, Ibrahimu na uzao wake hata milele. (K)
SHANGILIO: Lk.8:15
Aleluya, aleluya!
Wanabarikiwa wale walisikio
neno la Bwana na kulishika
Aleluya!
INJILI:
Bwana alimtokea lbrahimu karibu na mialoni ya Mamre, alipokuwa ameketi mlangoni pa hema yake mchana wakati wa hari, Akainua macho yake akaona, na tazama, watu watatu wamesimama mbele yake. Nave alipowaona alipiga mbio kuwalaki kutoka mlangoni pa hema, akainama mpaka nchi, akasema, Bwana wangu, kama nimeona fadhili machoni pako nakuomba usinipite sasa mimi mtumwa wako. Na yaletwe basi maji kidogo mkanawe miguu, mkapumzike chini ya mti huu. Nami nitaleta chakula kidogo, mkaburudishe moyo, baadaye mwendelee, iwapo mmemjia mtumwa wenu. Wakasema, Haya, fanya kama ulivyosema. Basi lbrahimu akaenda hima hemani kwa Sara, akasema, Himiza vipimo vitatu vya unga safi, uukande, ufanye mikate. lbrahimu akapiga mbio kwenda kundini, akaleta ndama wa ng’ombe aliye laini, mzuri, akampa mtumishi, naye akahimiza kuiandaa. Akatwaa siagi na maziwa, na ndama aliyoiandaa, akawaandikia mbele yao, akasimama karibu nao chini ya mti, nao wakala. Wakamwambia, Yu wapi Sara mkeo? Akasema, Yumo hemani. Akamwambia, Hakika nitakurudia wakati uu huu mwakani, na tazama, Sara mkeo atapata mwana wa kiume. Sara akasikia mlangoni pa hema iliyokuwapo nyuma yake. Basi lbrahimu na Sara walikuwa wazee, na umri wao mkubwa, na Sara alikuwa amekoma katika desturi ya wanawake. Kwa hiyo Sara akacheka moyoni mwake, akisema, Niwapo mkongwe, nitapata furaha, na bwana wangu mzee? Bwana akamwambia lbrahimu, Mbona Sara amecheka akisema, Mimi kweli nitazaa mwana, nami ni mzee? Kuna neno gani lililo gumu la kumshinda Bwana? Kwa muhula wake nitakurudia, wakati uu huu mwakani, na Sara atapata mwana wa kiume. Akakana Sara, akisema, Sikucheka, maana aliogopa. Naye akasema, Sivyo, umecheka.
WIMBO WA KATIKATI: Lk.1:46-50,53-55 (K)54
1. Moyo wangu wamwadhimisha Bwana. Na roho yangu imemfurahia Mungu Mwokozi wangu.
(K) Bwana alikumbuka rehema zake.
2. Unyonge wa mjakazi wake. Kwa maana, tazama, tokea sasa Vizazi vyote wataniita mbarikiwa. (K)
3. Kwa kuwa mwenye nguvu amenitendea makuu, Na jina lake ni takatifu. Na rehema zake hudumu vizazi hata vizazi, Kwa hao wanaomcha. (K)
4. Amemsaidia Israeli, mtumishi wake: Ili kukumbuka rehema zake. Kama alivyowaambia baba zetu, Ibrahimu na uzao wake hata milele. (K)
SHANGILIO: Lk.8:15
Aleluya, aleluya!
Wanabarikiwa wale walisikio
neno la Bwana na kulishika
Aleluya!
INJILI:
Mt.8:5–17
Yesu alipoingia Kapernaumu, akida mmoja alimjia, amsihi, akisema, Bwana, mtumishi wangu amelala nyumbani, mgonjwa wa kupooza, anaumwa sana. Yesu akamwambia, Nitakuja, nimponye. Yule akida akamjibu, akasema, Bwana, mimi sistahili wewe uingie chini ya dari yangu, lakini sema neno tu, na mtumishi wangu atapona. Kwa maana mimi nami ni mtu niliyewekwa chini ya mamlaka, mwenye askari chini yangu; nikimwambia huyu, Nenda, huenda; na huyu, Njoo, huja; na mtumwa wangu, Fanya hivi, hufanya. Yesu aliposikia hayo, alistaajabu, akawaambia wale waliomfuata, Amin, nawaambieni, Sijaona imani kubwa namna hii, kwa yeyote katika Israeli. Nami nawaambieni, ya kwamba wengi watakuja kutoka mashariki, na magharibi, nao wataketi pamoja na Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo katika ufalme wa mbinguni; bali wana wa ufalme watatupwa katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno. Naye Yesu akamwambia yule akida, Nenda zako; na iwe kwako kama ulivyoamini. Mtumishi wake akapona saa ile ile. Hata Yesu alipofika nyumbani kwa Petro, akamwona mkwewe Petro, mamaye mkewe, amelala kitandani hawezi homa. Akamgusa mkono, homa ikamwacha; naye akaondoka, akawatumikia. Hata kulipokuwa jioni, wakamletea wengi wenye pepo; akawatoa pepo kwa neno lake, akawaponya wote waliokuwa hawawezi, ili litimie lile neno lililonenwa na nabii Isaya, akisema, Mwenyewe aliutwaa udhaifu wetu, na kuyachukua magonjwa yetu.
MAOMBI
Ee Mungu, umetufunulia kuwa Wewe upo pia katika nafsi za wenzetu, hasa wale wanaohitaji msaada wetu. Kwa vile si rahisi kuwabaini wenye nia mbaya, twakuomba:-
Kiitikio: Upokee ombi letu.
1. Uwajalie viongozi wetu wa Kanisa imani thabiti, wapate kuwaokoa waamini wao dhidi ya yule mwovu, kwa neno lako na kwa kuadhimisha Sakramenti zako. Ee Bwana.
2. Uwajalie wote wenye mamlaka kukuogopa Wewe Mungu, na kuwahudumia walio chini yao kwa utu wema, na hivi kuheshimu uhuru wao na haki za kibinadamu. Ee Bwana.
3. Utuepushe na hila za yule mwovu katika harakati zetu za kutimiza amri ya kukupenda Wewe na jirani. Ee Bwana.
4. Wote wenye shida wasichoke kukukimbilia Wewe kwa sala; na uwajalie mahitaji yao yote. Ee Bwana.
5. Ndugu zetu wagonjwa waponywe kwa jina lako; na marehemu wote watakaswe dhambi zao na kuvikwa utukufu wa ufufuko huko mbinguni. Ee Bwana.
Tunaomba Mama yetu Bikira Maria azisindikize sala zetu. Kwa njia ya Kristo Bwana wetu. Amina.
Yesu alipoingia Kapernaumu, akida mmoja alimjia, amsihi, akisema, Bwana, mtumishi wangu amelala nyumbani, mgonjwa wa kupooza, anaumwa sana. Yesu akamwambia, Nitakuja, nimponye. Yule akida akamjibu, akasema, Bwana, mimi sistahili wewe uingie chini ya dari yangu, lakini sema neno tu, na mtumishi wangu atapona. Kwa maana mimi nami ni mtu niliyewekwa chini ya mamlaka, mwenye askari chini yangu; nikimwambia huyu, Nenda, huenda; na huyu, Njoo, huja; na mtumwa wangu, Fanya hivi, hufanya. Yesu aliposikia hayo, alistaajabu, akawaambia wale waliomfuata, Amin, nawaambieni, Sijaona imani kubwa namna hii, kwa yeyote katika Israeli. Nami nawaambieni, ya kwamba wengi watakuja kutoka mashariki, na magharibi, nao wataketi pamoja na Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo katika ufalme wa mbinguni; bali wana wa ufalme watatupwa katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno. Naye Yesu akamwambia yule akida, Nenda zako; na iwe kwako kama ulivyoamini. Mtumishi wake akapona saa ile ile. Hata Yesu alipofika nyumbani kwa Petro, akamwona mkwewe Petro, mamaye mkewe, amelala kitandani hawezi homa. Akamgusa mkono, homa ikamwacha; naye akaondoka, akawatumikia. Hata kulipokuwa jioni, wakamletea wengi wenye pepo; akawatoa pepo kwa neno lake, akawaponya wote waliokuwa hawawezi, ili litimie lile neno lililonenwa na nabii Isaya, akisema, Mwenyewe aliutwaa udhaifu wetu, na kuyachukua magonjwa yetu.
MAOMBI
Ee Mungu, umetufunulia kuwa Wewe upo pia katika nafsi za wenzetu, hasa wale wanaohitaji msaada wetu. Kwa vile si rahisi kuwabaini wenye nia mbaya, twakuomba:-
Kiitikio: Upokee ombi letu.
1. Uwajalie viongozi wetu wa Kanisa imani thabiti, wapate kuwaokoa waamini wao dhidi ya yule mwovu, kwa neno lako na kwa kuadhimisha Sakramenti zako. Ee Bwana.
2. Uwajalie wote wenye mamlaka kukuogopa Wewe Mungu, na kuwahudumia walio chini yao kwa utu wema, na hivi kuheshimu uhuru wao na haki za kibinadamu. Ee Bwana.
3. Utuepushe na hila za yule mwovu katika harakati zetu za kutimiza amri ya kukupenda Wewe na jirani. Ee Bwana.
4. Wote wenye shida wasichoke kukukimbilia Wewe kwa sala; na uwajalie mahitaji yao yote. Ee Bwana.
5. Ndugu zetu wagonjwa waponywe kwa jina lako; na marehemu wote watakaswe dhambi zao na kuvikwa utukufu wa ufufuko huko mbinguni. Ee Bwana.
Tunaomba Mama yetu Bikira Maria azisindikize sala zetu. Kwa njia ya Kristo Bwana wetu. Amina.
No comments
Post a Comment