MASOMO
ANTIFONA YA KUINGIA: Zab.48:9-10
Tumezitafakari fadhili zako, ee Mungu, katikati ya hekalu lako. Kama lilivyo jina lako, ee Mungu, ndivyo na sifa yako hata miisho ya dunia. Mkono wako wa kuume umejaa haki.
KOLEKTA:
Ee Mungu, kwa njia ya unyenyekevu wa Mwanao umeuinua ulimwengu uliokuwa umeanguka. Uwajalie waamini wako furaha takatifu ili, hao uliowaondoa katika utumwa wa dhambi, wapate kuifikia furaha ya milele. Kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo Mwanao, anayeishi na kutawala nawe katika umoja wa Roho Mtakatifu, Mungu, milele na milele.
SOMO 1:
ANTIFONA YA KUINGIA: Zab.48:9-10
Tumezitafakari fadhili zako, ee Mungu, katikati ya hekalu lako. Kama lilivyo jina lako, ee Mungu, ndivyo na sifa yako hata miisho ya dunia. Mkono wako wa kuume umejaa haki.
KOLEKTA:
Ee Mungu, kwa njia ya unyenyekevu wa Mwanao umeuinua ulimwengu uliokuwa umeanguka. Uwajalie waamini wako furaha takatifu ili, hao uliowaondoa katika utumwa wa dhambi, wapate kuifikia furaha ya milele. Kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo Mwanao, anayeishi na kutawala nawe katika umoja wa Roho Mtakatifu, Mungu, milele na milele.
SOMO 1:
Isa.66:10-14
Furahini pamoja na Yerusalemu, shangilieni kwa ajili yake, ninyi nyote mmpendao; furahini pamoja naye kwa furaha, ninyi nyote mliao kwa ajili yake; mpate kunyonya, na kushibishwa kwa maziwa ya faraja zake, mpate kukama, na kufurahiwa kwa wingi wa utukufu wake. Maana Bwana asema hivi, Tazama, nitamwelekezea amani kama mto, na utukufu wa mataifa kama kijito kifurikacho, nanyi mtapata kunyonya; mtabebwa; na juu ya magoti mtabembelezwa. Mfano wa mtu ambaye mama yake amfariji, ndivyo nitakavyowafariji ninyi; nanyi mtafarijiwa katika Yerusalemu. Nanyi mtaona, na mioyo yenu itafurahi, na mifupa yenu itasitawi kama majani mabichi; na mkono wa Bwana utajulikana, uwaelekeao watumishi wake.
WIMBO WA KATIKATI: Zab.66:1-7,16,20,(K)1
1. Mpigie Mungu kelele za shangwe, nchi yote,
Imbeni utukufu wa jina lake.
Tukuzeni sifa zake,
Mwambieni Mungu, Matendo yako yatisha kama nini!
(K) Mpigie Mungu kelele za shangwe,
nchi yote,
2. Nchi yote itakusujudia na kukuimbia,
Naam, italiimba jina lako.
Njoni yatazameni matendo ya Mungu,
Hutisha kwa mambo awatendayo wanadamu. (K)
3. Aligeuza bahari ikawa nchi kavu;
Katika mto walivuka kwa miguu;
Huko ndiko tuliko mfurahia,
Atawala kwa uweza wake milele. (K)
4. Njoni, sikieni, ninyi nyote mnaomcha Mungu,
Nami nitayatangaza aliyonitendea roho yangu.
Na ahimidiwe Mungu asiyeyakataa maombi yangu,
Wala kuniondolea fadhili zake. (K)
SOMO 2:
Furahini pamoja na Yerusalemu, shangilieni kwa ajili yake, ninyi nyote mmpendao; furahini pamoja naye kwa furaha, ninyi nyote mliao kwa ajili yake; mpate kunyonya, na kushibishwa kwa maziwa ya faraja zake, mpate kukama, na kufurahiwa kwa wingi wa utukufu wake. Maana Bwana asema hivi, Tazama, nitamwelekezea amani kama mto, na utukufu wa mataifa kama kijito kifurikacho, nanyi mtapata kunyonya; mtabebwa; na juu ya magoti mtabembelezwa. Mfano wa mtu ambaye mama yake amfariji, ndivyo nitakavyowafariji ninyi; nanyi mtafarijiwa katika Yerusalemu. Nanyi mtaona, na mioyo yenu itafurahi, na mifupa yenu itasitawi kama majani mabichi; na mkono wa Bwana utajulikana, uwaelekeao watumishi wake.
WIMBO WA KATIKATI: Zab.66:1-7,16,20,(K)1
1. Mpigie Mungu kelele za shangwe, nchi yote,
Imbeni utukufu wa jina lake.
Tukuzeni sifa zake,
Mwambieni Mungu, Matendo yako yatisha kama nini!
(K) Mpigie Mungu kelele za shangwe,
nchi yote,
2. Nchi yote itakusujudia na kukuimbia,
Naam, italiimba jina lako.
Njoni yatazameni matendo ya Mungu,
Hutisha kwa mambo awatendayo wanadamu. (K)
3. Aligeuza bahari ikawa nchi kavu;
Katika mto walivuka kwa miguu;
Huko ndiko tuliko mfurahia,
Atawala kwa uweza wake milele. (K)
4. Njoni, sikieni, ninyi nyote mnaomcha Mungu,
Nami nitayatangaza aliyonitendea roho yangu.
Na ahimidiwe Mungu asiyeyakataa maombi yangu,
Wala kuniondolea fadhili zake. (K)
SOMO 2:
Gal.6:14-18
Mimi, hasha, nisione fahari juu ya kitu chochote ila msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambao kwa huo ulimwengu umesulibishwa kwangu, na mimi kwa ulimwengu. Kwa sababu kutahiriwa si kitu, wala kutokutahiriwa, bali kiumbe kipya. Na wote watakaoenenda kwa kanuni hiyo, amani na iwe kwao na rehema, naam, kwa Israeli wa Mungu. Tangu sasa mtu asinitaabishe; kwa maana ninachukua mwilini mwangu chapa zake Yesu. Ndugu zangu, neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja na roho zenu. Amina.
SHANGILIO: Yn.1:12,14
Aleluya, aleluya!
Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu;
wote waliompokea aliwapa uwezo wa
kufanyika watoto wa Mungu.
Aleluya!
INJILI:
Mimi, hasha, nisione fahari juu ya kitu chochote ila msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambao kwa huo ulimwengu umesulibishwa kwangu, na mimi kwa ulimwengu. Kwa sababu kutahiriwa si kitu, wala kutokutahiriwa, bali kiumbe kipya. Na wote watakaoenenda kwa kanuni hiyo, amani na iwe kwao na rehema, naam, kwa Israeli wa Mungu. Tangu sasa mtu asinitaabishe; kwa maana ninachukua mwilini mwangu chapa zake Yesu. Ndugu zangu, neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja na roho zenu. Amina.
SHANGILIO: Yn.1:12,14
Aleluya, aleluya!
Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu;
wote waliompokea aliwapa uwezo wa
kufanyika watoto wa Mungu.
Aleluya!
INJILI:
Lk.10:1-12,17-20 (au somo fupi Lk.10:1-9)
Baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe. Akawaambia, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache; basi mwombeni Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi katika mavuno yake. Enendeni, angalieni, nawatuma kama wana kondoo kati ya mbwa-mwitu. Msichukue mfuko, wala mkoba, wala viatu; wala msimwamkie mtu njiani. Na nyumba yoyote mtakayoingia, semeni kwanza, Amani iwemo nyumbani humu; na akiwamo mwana wa amani, amani yenu itamkalia; la, hayumo, amani yenu itarudi kwenu. Basi, kaeni katika nyumba iyo hiyo, mkila na kunywa vya kwao; maana, mtenda kazi amestahili kupewa ujira wake. Msihamehame kutoka nyumba hii kwenda nyumba hii. Na mji wowote mtakaouingia, wakiwakaribisha, vileni vyakula viwekwavyo mbele yenu; wapozeni wagonjwa waliomo, waambieni, Ufalme wa Mungu umewakaribia.
(10:10-12,17-20) Na mji wowote mtakaouingia, nao hawawakaribishi, tokeni humo, nanyi mkipita katika njia zake semeni, Hata mavumbi ya mji wenu yaliyogandamana na miguu yetu tunayakung'uta juu yenu. Lakini jueni hili, ya kuwa Ufalme wa Mungu umekaribia. Nawaambia ya kwamba siku ile itakuwa rahisi zaidi Sodoma kuistahimili adhabu yake kuliko mji huo. Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako. Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme. Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru. Lakini, msifurahi kwa vile pepo wanavyowatii; bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.
MAOMBI
Bwana Yesu alitaka kuwatayarisha wasaidizi na kuwaita mitume atakaowatuma kuendeleza utume alioanzisha yeye mwenyewe. Aliwapa mitume wake maagizo mengi tuliyosikia katika Enjili ya leo. Baada ya kupaa mbinguni, Yesu aliwapelekea Roho wake ili awaimarishe kutimiza maagizo waliyopewa.
Ee Bwana Yesu,
1. Uliwapeleka mitume duniani ili watangaze habari ya Ufalme wa Mungu; uwaimarishe wote uliowachagua kwa utumishi wako.
2. Uliwaambia mitume wafuate njia uliyotangulia kuienda; utupe moyo tutegemee njia yako zaidi kuliko maarifa yetu ya kibinadamu.
3. Uliwatayarisha mitume wako waishi kadiri ya masharti ya Ufalme wa Mungu: utuwezeshe kuishi kadiri ya yale tunayoyatangaza.
4. Mitume wako walijaliwa amani wawashirikishe waumini. Utusaidie kueneza amani yako bila magomvi wala mafarakano.
5. Ulisema kwamba mti mwema unajulikana kwa matunda yake, utusaidie tuzalishe matendo mema kwa imani.
Ee Mungu Mwenyezi, uliweka mitume wawakusanye waumini wako. Uyasikilize maombi yetu tuwe waumini waaminifu kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Amina.
SALA YA KUOMBEA DHABIHU:
Ee Bwana, tunaomba sadaka tunayotoa kwa heshima ya jina lako itutakase, na ituwezeshe kutenda siku kwa siku kadiri ya uzima wa mbinguni. Kwa njia ya Kristo Bwana wetu.
ANTIFONA YA KOMUNYO: Zab.34:8
Onjeni mwone ya kuwa Bwana yu mwema; heri mtu yule anayemtumaini.
Au:
Mt.11:28
Bwana asema: Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
SALA BAADA YA KOMUNYO:
Ee Bwana, sisi tulioshibishwa na sadaka kubwa namna hii, tunakuomba utujalie kuitunza zawadi hiyo iletayo wokovu, wala tusiache kamwe kukusifu. Kwa njia ya Kristo Bwana wetu.
Baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe. Akawaambia, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache; basi mwombeni Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi katika mavuno yake. Enendeni, angalieni, nawatuma kama wana kondoo kati ya mbwa-mwitu. Msichukue mfuko, wala mkoba, wala viatu; wala msimwamkie mtu njiani. Na nyumba yoyote mtakayoingia, semeni kwanza, Amani iwemo nyumbani humu; na akiwamo mwana wa amani, amani yenu itamkalia; la, hayumo, amani yenu itarudi kwenu. Basi, kaeni katika nyumba iyo hiyo, mkila na kunywa vya kwao; maana, mtenda kazi amestahili kupewa ujira wake. Msihamehame kutoka nyumba hii kwenda nyumba hii. Na mji wowote mtakaouingia, wakiwakaribisha, vileni vyakula viwekwavyo mbele yenu; wapozeni wagonjwa waliomo, waambieni, Ufalme wa Mungu umewakaribia.
(10:10-12,17-20) Na mji wowote mtakaouingia, nao hawawakaribishi, tokeni humo, nanyi mkipita katika njia zake semeni, Hata mavumbi ya mji wenu yaliyogandamana na miguu yetu tunayakung'uta juu yenu. Lakini jueni hili, ya kuwa Ufalme wa Mungu umekaribia. Nawaambia ya kwamba siku ile itakuwa rahisi zaidi Sodoma kuistahimili adhabu yake kuliko mji huo. Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako. Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme. Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru. Lakini, msifurahi kwa vile pepo wanavyowatii; bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.
MAOMBI
Bwana Yesu alitaka kuwatayarisha wasaidizi na kuwaita mitume atakaowatuma kuendeleza utume alioanzisha yeye mwenyewe. Aliwapa mitume wake maagizo mengi tuliyosikia katika Enjili ya leo. Baada ya kupaa mbinguni, Yesu aliwapelekea Roho wake ili awaimarishe kutimiza maagizo waliyopewa.
Ee Bwana Yesu,
1. Uliwapeleka mitume duniani ili watangaze habari ya Ufalme wa Mungu; uwaimarishe wote uliowachagua kwa utumishi wako.
2. Uliwaambia mitume wafuate njia uliyotangulia kuienda; utupe moyo tutegemee njia yako zaidi kuliko maarifa yetu ya kibinadamu.
3. Uliwatayarisha mitume wako waishi kadiri ya masharti ya Ufalme wa Mungu: utuwezeshe kuishi kadiri ya yale tunayoyatangaza.
4. Mitume wako walijaliwa amani wawashirikishe waumini. Utusaidie kueneza amani yako bila magomvi wala mafarakano.
5. Ulisema kwamba mti mwema unajulikana kwa matunda yake, utusaidie tuzalishe matendo mema kwa imani.
Ee Mungu Mwenyezi, uliweka mitume wawakusanye waumini wako. Uyasikilize maombi yetu tuwe waumini waaminifu kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Amina.
SALA YA KUOMBEA DHABIHU:
Ee Bwana, tunaomba sadaka tunayotoa kwa heshima ya jina lako itutakase, na ituwezeshe kutenda siku kwa siku kadiri ya uzima wa mbinguni. Kwa njia ya Kristo Bwana wetu.
ANTIFONA YA KOMUNYO: Zab.34:8
Onjeni mwone ya kuwa Bwana yu mwema; heri mtu yule anayemtumaini.
Au:
Mt.11:28
Bwana asema: Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
SALA BAADA YA KOMUNYO:
Ee Bwana, sisi tulioshibishwa na sadaka kubwa namna hii, tunakuomba utujalie kuitunza zawadi hiyo iletayo wokovu, wala tusiache kamwe kukusifu. Kwa njia ya Kristo Bwana wetu.
No comments
Post a Comment